This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Tuesday, 31 December 2013

WATANGAZAJI 10 BORA WA RADIO STATIONS 2013 NDO HAWA KWA MUJIBU WA MTANDAO WA BONGO123.COM

Hivi Karibuni Tulifanya Mazungumzo Na Watangazaji Wakongwe Watatu Nchini, Godwin Gondwe Aka Double G Ambaye Kwa Sasa Ni Lecturer Wa Chuo Kikuu Cha Tumaini Na Pia Msomaji Wa Habari Wa ITV Na Shughuli Zingine, Sosthenes Ambakisye Aka SOS B Ambaye Kwa Sasa Hayupo Tena Kwenye Utangazaji Na Basil Mbakile Ambaye Kwa Sasa Ni Mtangazaji/Reporter Wa Idhaa Ya Kiswahili Ya BBC. Wote Hawa Kwangu Ni Miongoni Mwa Watu Walionivutia Kwenye Kazi Ya Utangazaji (Role Models) Na Niliwatafuta Kwa Lengo La Kutaka Kushare Nao Hofu Nilionayo Sasa Kwenye Vipindi Vya Burudani Katika Redio Nyingi Za Tanzania. Hofu Hiyo Ni Kuwa Kwa Mwaka 2013, Vipindi Vya Radio Vya Burudani Vimeshuka Kwa Kiasi Kikubwa Ukilinganisha Na Miaka Iliyopita. Kushuka Kwake Kunatokana Na Watangazaji Wengi Kufanya Kazi Kwa Mazoea, Kutojiandaa, Kukosa Vitu Exclusive Vya Kuweka Kwenye Vipindi Vyao, Udhaifu Katika Kufanya Interview Na Wasanii, Uchaguzi Wa Nyimbo Unaogubikwa Na Upendeleo Hasa Kwa Wasanii Wa Nyumbani Na Mambo Mengine. Wote Kwa Pamoja Walikiri Kuwepo Kwa Tatizo Hilo. Katika Maongezi Hayo Ambayo Mwakani Naweza Kuja Kuyaandikia Makala Maalum Kuhusiana Na Hilo, Godwin Gondwe Aliniambia Kuwa Watangazaji Wengi Wanatanguliza Umaarufu Badala Ya Bidii Ya Kazi. Alisema Watangazaji Wengi Hasa Wa Redio Kubwa Wamelewa Umaarufu Walionao Ambao Unawafanya Wasijitume Tena Kama Walivyokuwa Wakifanya Zamani. SOS B Alinieleza Kuwa Watangazaji Wa Sasa Hawajiandai Kabisa Na Hivyo Vipindi Vyao Kushindwa Kuwa Na Vitu Muhimu Vya Kuwalisha Wasikilizaji. Alimaanisha Kuwa, Vipindi Vingi Hukamilika Na Kumwacha Msikilizaji Bila Kitu Kinachoweza Kumuongezea Maarifa Au Elimu Mpya Kuhusu Burudani Na Wasanii Licha Ya Kuburudika. Basil Mbakile Alinieleza Kuwa Watangazaji Wengi Wanashindwa Kuwa Wabunifu Kwakuwa Wanakosa Mapenzi Ama ‘Passion’ Ya Utangazaji Na Hivyo Kuuchukulia Utangazaji Kama Ajira Kumpatia Tu Ujira. Pamoja Na Hofu Hiyo Wapo Watangazaji Wa Radio Wanaoendelea Kujituma Kuvifanya Vpindi Vyao Viwe Bora Zaidi. Kwa Mwaka 2013, Hawa Ni Watangazaji Bora Zaidi Upande Wangu Na Ambao Naamini Wataongeza Bidii Zaidi Mwaka 2014 Ili Wawe Bora Kupita Walivyokuwa Mwaka 2013. 1. Millard Ayo – Amplifaya Na Clouds FM Top 20 IMG_2490 Kwangu Na Kwa Wengine Wengi, Millard Ayo Ndio Mtangazaji Bora Zaidi Tanzania Kwa Sasa. Kwa Miaka Miwili Mfululizo, 2012 Na 2013, Millard Amekuwa Akiongoza Kura Za Maoni Za Bongo5 Kuhusu Mtangazaji Anayesikilizwa Zaidi Tanzania. Godwin Gondwe Anamchukulia Millard Kama Mtangazaji Anayejituma Zaidi Kuliko Wote Tanzania Na Kwamba Kama Angekuwa Anafanya Kipindi Muda Sawa Na Yeye, Basi Angekuwa Anampa Hofu Sana. Naye Mtangazaji Mkongwe, Masoud Masoud Wa TBC Taifa, Aliwahi Kusema Kwenye Kipindi Cha Mkasi Mwaka Huu Kuwa, Millard Ndiye Mtangazaji Anayemkubali Kwa Sasa Na Humkumbusha Enzi Zake Za Ujana Wake. Japo Si Kituo Chake Cha Kwanza Kuanza Kazi, Jina La Millard Lilianza Kufahamika Nchini Kupitia Kipindi Cha Milazo 101 Cha Radio One. Sauti Yake Yenye Mamlaka Na Ubunifu Hewani, Ulikifanya Kipindi Hicho Kuwa Maarufu Kuliko Vingine Vya Burudani Katika Radio Hiyo Inayomilikiwa Na Kampuni Ya IPP. Kuondoka Kwake Radio One Kulikuwa Ni Pigo Kubwa Lakini Lenye Neema Kwa Clouds FM. Alihamia Clouds FM Na Kuanzisha Kipindi Kipya Kiitwacho Amplifanya Ambacho Kilichukua Nafasi Ya Kipindi Cha Nyimbo Za Kiafrika, Bambataa. Haikuchukua Muda Kipindi Cha Amplifanya Kikawa Miongoni Mwa Vipindi Bora Kabisa Clouds FM. Kipindi Hicho Pia Ni Miongoni Mwa Vipindi Vinavyoiingizia Fedha Nyingi Redio Hiyo Na Kumfanya Millard Kuwa Miongoni Mwa Watangazaji Wa Kituo Hicho Wanaolipwa Mshahara Mkubwa Zaidi. Leo Hii Millard Ni Miongoni Mwa Watangazaji Bora Tanzania Na Wanaosikilizwa Zaidi. Si Maarufu Tu Redioni Bali Pia Ndiye Mtangazaji Wa Tanzania Mwenye Mashabiki Wengi Zaidi Kwenye Mitandao Ya Kijamii. Ana Zaidi Ya Followers 75,000 Kwenye Twitter Huku Facebook Akiwa Na Likes Zaidi Ya 153,000.Umaarufu Wake Kwenye Mitandao Ya Kijamii Umemfanya Ageuke Brand Na Kuyavutia Makampuni Makubwa Kama CRDB Bank, Fast Jet Na Mengine Kudhamini Kile Anachotweet. Tweets Zake Tu Zinamuingizia Fedha Huku Akimiliki Pia Website Yake Binafsi Yenye Wasomaji Lukuki Na Yenye Matangazo Mengi. Kwa Mshahara Anaoupata, Kazi Ya Uripota Wa DSTV, Ubalozi Wa Fastjet, Website Yake, Deal Za Voice-Overs Na Mambo Mengine, Millard Anaingiza Takriban Ama Zaidi Ya Shilingi Milioni 10 Kila Mwezi.Millard Ni Zaidi Ya Mtangazaji, Bali Ni Mwandishi Mwenye ‘Pua Ya Habari’ (Nose For News) Huku Akiongoza Kwa Kuja Na Angle Za Kipekee Za Habari Zenye Mvuto Kwa Watu (Human Interest Stories) Zinazokifanya Kipindi Chake Cha Amplifaya Kuteka Matangazo Ya Jioni Siku Za Wiki. Pamoja Na Kupata Mafanikio Hayo, Millard Ameendelea Kuwa Mchapakazi, Simple, Mtu Anayejituma Kutafuta Habari Hata Sehemu Za Mbali Kabisa, Mcheshi Na Mtu Wa Watu. Hakuna Shaka Kuwa, Millard Ana Mustakabali Wa Nguvu Kwenye Fani Hiyo. Ni Mfano Wa Kuigwa Kwa Watangazaji Wengine Na Hazina Kubwa Kwa Wazazi Wake, Clouds Media Group Na Hata Taifa Kwa Ujumla. 2. Hamis Mandi Aka B12 – XXL Clouds FM B12 Kwa Muda Mrefu, XXL Kimeendelea Kuwa Kipindi Namba 1 Cha Burudani Nchini. Kama Wimbo Wa Msanii Usipochezwa Kwenye XXL, Basi Wimbo Huo Una Kasoro. Yeye Mwenyewe B-Dozen Anajiita Mfalme Wa Vipindi Vya Mchana Na Hakuna Msanii Yeyote Mkubwa Wa Bongo Ambaye Hajawahi Kuhojiwa Na Mtangazaji Huyu Mahiri. Kwangu Mimi, B-Dozen Ndio Roho Ya XXL Ambaye Kama Asipokuwepo, Hakuna Mtangazaji Anayeweza Kukipa Kipindi Hicho Ladha Iliyozoeleka. Ndicho Kipindi Ambacho Nyimbo Kali Za Wasanii Zimezinduliwa Exclusively Mwaka 2013. Mwaka Huu B12 Alitajwa Kwenye Orodha Ya TopTen Most Ya Channel O Ya Watangazaji Bora Wa Afrika Huku Yeye Akikamata Nafasi Ya 9.3. Raheem Da Prince – The Switch, Times FM Raheem Utangazaji Wa Raheem Na Uelewa Wake Wa Muziki, Hunifanya Nivutike Sana Kusikiliza Kipindi Chake Cha The Switch Kila Jumamosi. Japokuwa Madj Wa Show Hiyo DJ D-Ommy Na DJ KU Ni Sehemu Ya Kivutio Cha Show Hiyo, Ufuatiliaji Wa Raheem Kuhusiana Na Muziki Wa Marekani Na Kwingine, Hunifanya Nitoke Na Elimu Kubwa Kila Nisikilizapo Show Yake. Amekuwa Akijituma Sana Kuchambua Matukio Ya Muziki Yakiwemo Kuchambua Album Za Wasanii Wa Marekani Na Mambo Mengine. Mwaka Huu Nilifurahia Zaidi Uchambuzi Alioufanya Kwa Kushirikiana Na Reuben Ndege Aka Nchakalih, Hermy B Na Miss East Africa 2012, Jocelyne Maro Wa Album Ya Jay Z, Magna Carta Holy Grail. Sijawahi Kusikia Uchambuzi Mkali Wa Muziki Kama Huo Kwenye Redio Yoyoye Ya Tanzania Kwa Miaka Mingi. 4. Vanessa Mdee – The Hitlist, Choice FM 308042_481355628565126_1797969664_n  


Vanessa Mdee hutangaza kipindi cha The Hitlist cha Choice FM na ndio sehemu yangu iliyosalia ya kusikiliza nyimbo mpya za Marekani ambazo kwa sasa ni nadra kuzikisia kwingine. Awali show niliyokuwa nikiitegemea kwa kusikiliza selection nzuri ya nyimbo mpya za Marekani ilikuwa ni kwenye The Cruise ya Choice FM kipindi ambacho Steve Kabuye alikuwa anatangaza bado. Napenda uchangamfu wa Vee Money kwenye show yake na uelewa mzuri wa ngoma za nje. 5. Jabir Saleh – The Jump Off, Times FM JabirNamchukulia Jabir Saleh aka Kuvikacha kama maktaba ya muziki wa vijana. Nadiriki kusema ni watangazaji wachache sana Tanzania wenye uelewa wa muziki wa Hip Hop kama alionao Jabir. Ukisikiliza kipindi cha The Jump Off, hakuna shaka kuwa elimu yako kuhusu Hip Hop itapanuka zaidi na kamwe huwezi kujuta kumsikiliza. 6. Sam Misago – Power Jams , EA Radio 944577_346691582123045_1523449421_n Power Jams na XXL ndivyo vipindi vyenye ushindani zaidi kwa siku nyingi katika vipindi vya mchana. Akiwa amejipa jina ‘The Presenter’s President, Sam ni miongoni mwa watangazaji wenye mashabiki wengi mchana. 7. Bizzo – Show Time; New Chapter , RFA1239763_570266786344526_1898720372_n Umaarufu wa Bizzo ulianzia Ebony FM, Iringa ambako alikuwa akifanya show iitwayo The Splash. Kwa sasa Bizzo ambaye jina lake halisi ni Renatus Kiluvya, ni mtangazaji wa kipindi cha Show Time cha Radio Free Africa. Kwa kiasi kikubwa amejitahidi kuliziba pengo la Kidbwoy aliyekuwa amezoeleka sana kwenye kipindi hicho. 8. Perfect Crispin – Club 10, Clouds FM perfect 

Perfect ni mtangazaji wa kipindi cha vijana hususan wa sekondari cha Club 10. Ni kipindi maarufu zaidi kwa wanafunzi wa sekondari kuliko vyote nchini na kwa kiasi kikubwa ameendelea kukimudu na kukiendesha kwa ustadi mkubwa mwaka 2013. 9. Jimmy Jamal – Daladala Beat, Magic FM 1236110_708050345876973_748240325_n Dala Dala Beat ni miongoni mwa show kongwe kabisa za burudani nchini. Jimmy ni mtangazaji mwenye sauti nzito na mwenye uelewa mkubwa wa muziki wa ndani na nje. Napenda namna anavyofanya interview zake na uchangamfu hewani. 10. King David King Davidy  
Kwa wengi, King David ni jina geni kabisa. Lakini kitu kimoja cha uhakika kuhusu jamaa huyu ni kwamba ukimsikiliza lazima utamkubali na kama angekuwa anatangaza redio kubwa, kwa sasa angekuwa akicheza ligi moja na watangazaji wengi hao juu. Ana sauti nzuri na yenye mamlaka, anajua muziki wa ndani na nje na ni mbunifu. Alikuwa mtangazaji wa Uplands FM ya Njombe ambako alikuwa akifanya vipindi kama Bonge la Drive na Uplands FM Top 20 na kwa sasa amehamia kwenye kituo cha redio kipya kiitwacho Kings FM cha Njombe kitakachoanza rasmi matangazo mwakani

Wednesday, 4 December 2013

Hot Newz Daily: TAZAMA PICHA HIZI ZITAKAZO KUSHANGAZA NA KUKUFURAH...

Hot Newz Daily: TAZAMA PICHA HIZI ZITAKAZO KUSHANGAZA NA KUKUFURAH...:  Photograph by CAROLYN KASTER (via  The Atlantic: In Focus )

: TAZAMA PICHA HIZI ZITAKAZO KUSHANGAZA NA KUKUFURAH...

Hot Newz Daily: TAZAMA PICHA HIZI ZITAKAZO KUSHANGAZA NA KUKUFURAH...:  Photograph by CAROLYN KASTER (via  The Atlantic: In Focus )

Tuesday, 1 October 2013

MAAJABU MTOTO WA MIAKA MIWILI ASHIKA MIMBA

article-2439498-1869504E00000578-235_634x416Mtoto wa miaka miwili wa Huaxi nchini China, amefanyiwa upasuaji wa kujifungua baada ya madaktari kugundua kuwa alikuwa na mimba.Xiao Feng, alipelekwa hospitali baada ya tumbo lake kuwa kubwa kiasi ambacho alijikuta akishindwa kupumua.


Alipolazwa, madaktari walichukua picha za x-rays na MRI ba kugundua kuwa Feng alikuwa amebaba mimba isiyokua na hivyo kuamua kumfanyia upasuaji.
Waliiondoa mimba hiyo changa iliyokuwa na upana wa cm 20 na tayari ilikuwa imeanza kuwa vidole. Mimba hiyo ilitakuwa kuwa pacha wa mtoto huyo. Pacha huyo wa sponji angekua na kuwa mtoto wa kiume.

article-2439498-1869A2B000000578-917_634x431                         Feng akiwa  amebebwa na mama yake baada ya upasuaji
Mapacha wanaofanana hutokea pale yai linapojigawa wakati wa urutubishaji na mapacha walioungana hutokea pale yai linaposhindwa kujigawa. 

Monday, 30 September 2013

TAARIFA INAYOSEMA HUENDA MAGAIDI WA WESTGATE WALITOROKEA NJIA YA MAJI TAKA CHINI YA JENGO HII HAPA


Wakati bado kuna maswali mengi kuhusu magaidi waliohusika na shambulio la Westgate kama kweli waliuawa kama isemavyo taarifa ya serikali ya Kenya, mtandao wa Mirror umetoa taarifa kuhusu tetesi za uwezekano wa magaidi hao kutorokea njia ya maji taka kutoka katika jengo hilo.

Mtandao huo umedai kuwa baadhi ya magaidi walitoroka kupitia njia ya maji taka iliyoko chini ya jengo la Westgate inayoenda kutokea katika mto Nairobi.

Kwa mujibu wa habari hiyo njia hiyo inaanzia eneo la maegesho ya magari katika jengo la Westgate na inaenda moja kwa moja kutokea katikati ya jiji la Nairobi. Magaidi hao wanahofiwa kutumia njia hiyo ya maji taka kutoroka na kuwaacha wengine wakiendelea kushambulia.


Taarifa hiyo inaendelea kudai kuwa wana usalama wanadai kuwa magaidi wa Al-shabaab walisafiri umbali wa nusu maili kwa magoti katika njia hiyo ya chini ya ardhi katika njia ya maji taka.

Chanzo kimoja kilisema “They escaped like sewer rats. The terrorists would have been able to pass through the underground tunnels at a rapid pace and surface almost unnoticed”.

Taarifa hiyo inaendelea kusema kuwa wachunguzi wa Kenya hawakuigundua njia hiyo ya kutorokea mpaka masaa 72 kupita baada ya shambulio kutokea.

Sheikh Azzan: “Viongozi wawe waadilifu”

                                                                  Picha hii ya mwezi Juni 2012 inawaonesha viongozi wa Jumuiya ya Uamsho ambao hivi sasa wako ndani . Kutoka kulia ni Sheikh Azzan Hamdan (kulia, ametolewa kwa dhamana ya matibabu), Sheikh Farid Hadi na Maalim Mussa Juma (bado wako ndani).                                                                                                                           MAPEMA Jumamosi asubuhi Sheikh Azzan Khalid Hamdan, kiongozi mwandamizi wa Jumuiya ya 
Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu, alizungumza na Zanzibar Daima Online nyumbani kwake Mfenesini, Unguja.
Na Ahmed Rajab
ALIITIKIA simu yangu kwa upole na unyenyekevu bila ya kukasirika kwamba nilimsumbua kwa simu mara tu baada ya swala ya alfajiri.  Nilimwambia niko tayari kwenda aliko ili tuzungumze. Hakunikatalia.
Alinielekeza kwamba tukishafika kwenye Mahakama ya Mfenesini tutazikuta nyumba zake nyuma ya maduka.  Kulikuwa kumekwishapambazuka nilipowasili na mwenzangu na majirani zake Sheikh Azzan waliojaa bashasha walitusalimia vizuri na kutuonyesha nyumba zake mbili.
Tuliposogea karibu watu wake wa nyumbani walituambia ni ipi kati ya hizo mbili alimokuwamo Sheikh Azzan.  Tulimkuta amekaa chini na hakuweza kusimama kutusalimia kwa maumivu yanayosababishwa na mawe kwenye mafigo yake.
Alitutaka radhi mara mbilimbili kwani alihisi alifanya utomvu wa adabu kutusalimia bila ya kusimama.
Alizidi kunitaka radhi kwani tulikuwa tumepanga tukutane jana Magharibi nikafika tulikoagana lakini sikumkuta.
azzan1
Sheikh Azzan Khalid Hamdan ambaye kwa sasa yuko nje kwa dhamana ya matibabu.
“Watu wengi sana walikuwa wakija kiasi cha kunifanya nichanganyikiwe na nikasahau kama tuliagana,” Sheikh Azzan alinambia.
Hao watu wengi walikuwa wakienda kumpa ‘stahil salama’ kwani saa chache tu kabla hapo jana (Ijumaa) Jaji Mkuu Omar Othman Makungu akiwa katika Mahakama ya Vuga aliamua kuwa Sheikh Azzan aachiwe kwa dhamana ili aweze kwenda ng’ambo kwa matibabu.
Sheikh Azzan mwenyewe hakuwako Mahakamani wala hakuwepo gerezani alikokuwa ameshikwa pamoja na viongozi wengine wa Uamsho. Alikuwa bado amelazwa kwenye Spitali ya Mnazi Mmoja.
Tukiyaacha mawe katika figo zake, Sheikh Azzan anatatizwa pia na ukosefu wa usingizi.
“Sipati usingizi usiku wala mchana.  Pia nina ulcer na mara nyingi hukimbilia spitali.  Nimepoteza fahamu mara tano — mara mbili gerezani na mara tatu spitali,” alisema Sheikh Azzan.
Nilimuuliza kuhusu hali za wenzake waliobaki gerezani.
“Wazima isipokuwa wana matatizo madogo madogo ya kiafya,” alisema Sheikh Azzan anayetarajia kwenda India kwa matibabu Jumanne ijayo.
Akieleza hali za gerezani za wafungwa wenzake, Sheikh Azzan alisema kwamba wanaachiwa kuwa pamoja.  Watu kumi wanaswali pamoja swala za adhuhuri na alasiri.
“Swala za isha, maghribi na alfajiri huswaliwa na watu watatu watatu,” alisema Sheikh Azzan na akaongeza kuwa kuna mtu mmoja, Mzee Suleiman Juma.
Je, alipata fununu yoyote kwamba ataachiwa jana?
“Nilikuwa na tamaa lakini nilishangaa nilipoona kwamba masharti si magumu ni ya kawaida”, alieleza Sheikh Azzan.
Hata hivyo, siku hizi kwa mujibu wa Sheikh Azzan hali ya mambo gerezani imebadilika kidogo.  Yeye na wenzake wamekuwa wakiruhusiwa kupata chakula kutoka makwao pamoja na magazeti.
“Tuna nafuu kubwa sio kama mwanzo.  Zamani tukiwekwa katika mazingira ya kila mtu abakie chumbani mwake kwa muda wa siku 42,” alisema Sheikh Azzan.
Aliongeza kusema siku hizi wao wafungwa wana maelewano mazuri na watu wa magereza na kwamba hao watu wa magereza, kwa hakika, wanasaidia sana.
Sheikh Azzan aliyakhitimisha mazungumzo yetu kwa kuwashukuru Wazanzibari na Waislamu wote, kwa jumla, kwa kuwa pamoja nao viongozi wa Uamsho walio korokoroni.  Aliwasihi waendelee kumuombea dua.
Watu wengi, alisema, wamejitolea kumsaidia kugharimia matibabu yake huko India.  Inavyosemekana ni kwamba zinahitajiwa shilingi milioni 16 kwa matibabu hayo.
Sheikh Azzan alikuwa na ujumbe maalum kwa viongozi wa Serikali.  Alisema viongozi hao wanapaswa wawe waadilifu.
“Sisi raia wa kawaida na wa halali.  Hatukatai kushtakiwa lakini watufanyie uadilifu.  Tunaiomba Serikali iharakishe hii kesi.  Muda umekwishakuiwa mkubwa.  Mheshimiwa Rais [Ali Mohamed Shein] alikula kiapo kuwa atakuwa mwadilifu basi awe mwadilifu,” alisihi Sheikh Azzan.
“Kwa upande mwingine naishukuru Serikali kwa kulifikiria ombi langu na Mahakama kwa kutenda uadilifu kwa kutoniwekea pingamizi,” alimaliza Sheikh Azzan.
Kesi ya washtakiwa wa Uamsho inatarajiwa kusikilizwa tena Oktoba 7.

Saturday, 28 September 2013

BongoClan™ : BREAKING NEWZ: SERIKALI YAYAFUNGIA MAGAZETI YA MWANANCHI NA MTANZANIA

TAMKO LA SERIKALI Serikali imeyafungia kutochapishwa Magazeti ya MWANANCHI na MTANZANIA kuanzia 27 Septemba,2013 kutokana na mwenendo wa magazeti hayo kuandika habari na makala za uchochezi na uhasama kwa nia ya kusababisha wananchi wakose imani kwa vyombo vya dola hivyo kuhatarisha amani na mshikamano ulipo nchini. Gazeti la MWANANCHI limefungiwa kutochapishwa kwa siku kumi na nne(14) kuanzia 27 Septemba,2013.Adhabu hii imetangazwa k... more »

BongoClan™ : TAZAMA PICHA YA SHOW YA DIAMOND ALIYOFANYA JANA ZANZIBAR JINSI ILIVYOJAZA


Haya ndiyo aliyoyasema Diamond Platnumz kwa fan wake wa Zanzibar Oooh Zanzibar, u got me speechless, I dont even know how to start thanking you, or show my appreciations for the love and support that You have for me..I'm OVER JOYED..surely! Truly! You guys are my no.1 fans... The love I have for you is beyond measure, beyond words that I can explain.. Out of this sphere!.. Zanzibar! I love you u guys very very very !!MUCH. Thank U

BongoClan™ : WASANII 10 WA BONGO FLAVA WALIOINGIZA PESA NYINGI ZAIDI 2013 KWA MUJIBU WA BONGO 5

Biashara ya muziki Tanzania imeendelea kupanuka kwa kiasi kikubwa, na wasanii wenye hits, majina, connection, bahati na sababu zingine wameendelea kuingiza fedha nyingi kutokana na muziki wao. Njia kubwa na za uhakika zinazowapatia mapato wasanii ni pamoja na malipo ya show, malipo ya ringtones, endorsements (mfano kuwa mabalozi wa brands mbalimbali na kufanya matangazo) na wengine kupata kipato kupitia biashara walizozianzisha.hii hapa ndio listy ya wasani waliongiza pesa nyingi
DIAMOND 1
ANACONDA 2
AY 3
4 DIMPOZI
5 MADEE
     6     MWANA AF
cHEGE 9

                                                           PRO 9






NEY 9                                                                           
                                                                     temba wa 10




























































Sunday, 8 September 2013


yoooooo



Saturday, 7 September 2013

mzee duchi

oyoooooooooooooooooooooooooooo`

Thursday, 5 September 2013

duchi